MABISHANO KATI YA MWALIMU NA MWANAFUNZI JUU YA UWEPO WA DUNIA ZAIDI YA MOJA



Mwalimu mmoja wa Somo la Sayansi katika Shule ya Msingi Mtakuja alijikuta katika mdahalo mkubwa baada ya kutofautiana kifikra na mwanafunzi wake. Hii ilijitokeza baada ya Mwalimu huyo kufundisha uwepo wa sayari tisa na kuthibitisha kuwa ndani ya sayari zote zilizobainishwa kijeografia, Dunia iko moja tu.
“wanafunzi wangu, nataka mjue hili, yapo mafundisho mengi yanayoonyesha kuwa kunauwepo wa Dunia nyingine. Binafsi nisingependa mshikamane sana na mafundisho hayo mpaka yatakapokuwa yamethibitishwa.” Alisema Mwalimu Yule huku akigeuka kumtizama mwanafunzi aliyekuwa akinyoosha mkono ishara ya kuomba kuchangia mada.
“eeh, Juma unalipi la kuongea , au unaswali”alisema mwalimu.
“hapana mwalimu mimi sina swali ila ninataka kujenga hoja kuthibitisha kuwa kunauwepo wa Dunia zaidi ya moja”alisema Mwanafunzi Juma.
“kijana usijichanganye,nakupa nafasi ya kuchangia lakini usije ukathubutu kusema kuwa kuna Dunia zaidi ya moja kwenye Mtihani”alisema Mwalimu.
“Mwalimu, kijeografia ni kweli kwamba Dunia iko moja tu ,ila kimantiki ninadhani Kuna Dunia zaidi ya moja”alisema Juma.
“hebu tuelezee”alisema mwalimu.
“Mwalimu, Dunia ya pili ninayoisema watu wakaao ndani yake kwa asilimia kubwa ni watu wanaoishi maisha yasiyo yao,huko watu hawazaliwi bali wanajisajili ili kuweza kuishi. Watu wanaishi kwenye Dunia hiyo kutegemea uwepo wa Dunia hii tunayokaa, nikimaanisha bila ya uwepo wa Dunia hii basin a Dunia yao isingekuwepo. Cha kushangaza ni kwamba hata majina wanayotumia Duniani huko sio majina halisi waliyopewa na Wazazi wao,kama huku kwenye Dunia yetu mtu anaitwa Denis Kezirahabi Machovu, basi kule atajiita DK. Machovu jr. Kwenye Dunia hiyo karibia kila mtu anamiliki kampuni maana ukitizama usajili wao utakuta kila mtu kwenye nafasi ya kujaza kazi anayoyanya utakuta ameweka yeye ni C.E.O mahali Fulani. Katika Dunia hii pumzi inayohitajika ni Data zako tu, vinginevyo utajua tu mtu Fulani kaongea neon Fulani bila kuona nyuso yake. Huko nako kuna maofisi kwani watu wa Dunia yetu hii wameingia huko na kuamua kufanya biasharakwenye ulimwengu huo mwingine”alisema Juma na kisha akaketi.
Wanafunzi wengi walimpigia makofi huku wakistaajabu juu ya weledi wake wa kutumia fasihi ili kuonyesha ujumbe alionao.Mwalimu naye alibaki ameduwa kwani alishangazwa sana na ujumbe ule kwakuwa hata yeye kwenye Dunia hiyo nyingine anajulikana kama mmiliki wa kampuni Fulani kitu ambacho si kweli, Mwalimu alitoa noti ya shilingi Elfu Kumi na kumpatia Juma kama zawadi huku akimsihi asitumie Nadharia ile katika sehemu yoyote ihusianayo na masomo yake.
Imeandikwa na Lameck Mugisha




Comments