MICHEZO:Mfahamu Mwanasarakasi mdogo kutoka Kenya aliyekutana na Raisi wengi.



   Sura na muonekano wake ni mithiri ya mtoto mtulivu sana, najua wengi kwakumuona na bila ya kumfahamu usingewezxa kudhani kama anauwezo wa kuruka japo kwa umbali wa sentimita moja kwenda juu. Si wa kujiweka sana ukurasa wa mbele, bali kazi na maajabu anayofanya kwaajili ya taifa lake ndivyo vinavyo mfanya afahamike sana hapa kwetu Afrika mpaka Mabala ya nje.
 
    Wendy Waeni ni Mwanasarakasi mdogo kutoka nchini Kenya, inasemekana kwa wengi kuwa pengine ndiye mwanasarakasi mdogo zaidi Afrika mwenye jina kubwa ndani na nje ya Bara la Afrika.Wendy Waeni hadi alipofikisha miaka kumi  tayari alikuwa amekwisha perfom mbele ya maraisi wengi sana kutoka ndani na nje ya Afrika,Paul Kagame, John Mahama, Uhuru Kenyata na David Cameron ni Miongoni mwa viongozi ambao Wendy amewahi kuwaonyesha kipawa alichonacho cha kucheza sarakasi.
    Uwezo wa Wendy ulianza kuonekana tangu akiwa Mdogo sana, na kwa wanaomfahamu wanasema alikuwa akifanya michezo ambayo iliwatisha wengi hususan mama yake mzazi. Mtoto huyu kipaji chake kiliendelea kukua siku hadi siku hali iliyopelekea kujiunga katika kikundi cha HURUMA, kinacholea vipaji vya aina hiyo.
     Baada ya Wendy kujiunga katika kundi hilo lililokuwa likiitwa kwenye maonyesho kadha wa kadha, ndipo taifa la Kenya lilipomtambua na kuona uwezo aliokuwanao mtoto huyu kwani amekuwa kivutio kwa wengi pindi alipofanya maonyesho katika sherehe nyingi za kitaifa.
     Siku kadhaa zikapita, Jeff koinange pamoja na Television nyingi kutoka Kenya zilizizima kwa uwezo aliokuwanao binti huyu, interviews nyingi zilipelekea Wendy Waeni kujulikana mpaka kimataifa. Lakini kati ya ndoto alizo kuwanazo, ni kufanya maonesho mbele ya Rais wa Rwanda Paul Kagame, na ndoto yake ilitimia miaka miwili baadaye ambapo alialikwa na Rahis huyo kwenda white house ya Rwanda.
     Hatimaye ndoto yake ikatimia, na hakuishi tena ndani ya ndoto, bali aliutembelea uhalisia wake.


Imeandikwa na
L.A.Mugisha
0742549200

Comments