MEACULPA MEACULPA



                                MEA CULPA MEA CULPA MEA MAXIMA CULPA
                           (NIMEKOSA MIMI NIMEKOSA MIMI NIMEKOSA SANA)

Basi katika nchi za ulaya hadithi nyingi zilitapakaa, Makala nyingi zikachapwa na waandishi mahiri waliobobea katika fani hiyo, wote wakijaribu kusema kile wanachokijua kuhusu Nchi yenye mashimo tu, na mashimo hayo yanauwezo wa kuongea.
Mwalimu Jones Fernandes katika kitabu chake cha WONDERS OF THE TALKING HOLE, alijaribu kuelezea kile anachokijua kuhusu nchi iliyojaa mashimo yenye uwezo wa kunena,alisema pengine ni mabaki ya miili ya watu wa kale yamejumuika na kutengeneza uhai wa kiumbe kisicho onekana kiishicho ndani ya mashimo hayo.
Mchunguzi wa maswala ya miamba kutoka uingereza bwana Peter schzech naye alikaliliwa akisema pengine ni miamba iliyoko chini ya ardhi imekuwa ikisuguana na hivyo basi kupelekea sauti ikasikika kutoka katika mashimo yale ambayo hayajulikani yalichimbwa na nani na kwa kusudi gani kwani ni ya muda mrefu sana.
Swala hili lilichukuliwa kwa uzito na wanafunzi kutoka chuo kikuu cha OXFORD Ambao waliamua kwenda kufanya uchunguzi juuu ya nchi ya mashimo yanayoongea, walipofika kule walishangazwa sana, nchi zima yalijaa mashimo tu wasingeweza kutembea kilomita moja bila ya kukutana na shimo kubwa sana, na kilichowashitua zaidi ni kwamba kulikuwa na sauti zilizosikika kutoka katika mashimo yale zikisema “MEA CULPA MEA CULPA MEA MAXIMA CULPA”maneno ya kilatini yenye maana sawa na “NIMEKOSA MIMI NIMEKOSA MIMI NIMEKOSA SANA” Hakika walishangazwa na sehemu ile, kwani hakukuwa na Binadamu wa aina yoyote ile.

Basi watafiti wale walikaza moyo na kujitosa kuingia katika mashimo yale ikiwa ni moja ya mbinu ili waweze kutambua chanzo cha sauti ile,ili wagarimu masaa kadhaa mpaka kufika ndani kabisa ya mashimo yale, kule walishangaa walichokiona, waliwaona wazee na vikongwe wakisujudu mbele ya vijana na watoto wadogo huku wakisema kwapamoja MEA CULPA MEA CULPA MEA MAXIMA CULPA(NIMEKOSA MIMI NIMEKOSA MIMI NIMEKOSA SANA), wazungu wale walishangazwa na jamii ile kwani walikuwa ni watu masikini sana, hakuna mtu hata mmoja aliyekuwa amevalia nguo isiyo na tundu, wote walionekana kuwa wachafu. Vijana walikuwa wameshikilia fimbo za mikwaju huku wakiwacharaza wazee wale ambao walikuwa wakiendelea kusujudu mbele yao wakisema nimekosa mimi nimekosa mimi nimekosa sana.

Wazungu wale walijaribu kuwauliza vijana wale na watoto wale ni kwanini wanawacharaza vile babu na bibi zao,wale vijana waliwaangalia wazungu wale kwa jaziba nyingi huku wakionyesha kuwa sio watu wema sana kwao.kijana mmoja kati ya wale alitoka mbele na kuanza kusema huku akilia sana………….
“Ni bora mmekuja ninyi, maana napo wangekuja babazenu bado tungewaunganisha na kuwaadhibu kwa pamoja bila ya kujali wadhifa wao, hawamnao waona ni mabepari wanchi hii myaka kadhaa iliyopita, ni baba na babu zetu. Tumekuwa tukiwauliza ni kwanini tunaishi kwenye mashimo kwa muda mrefu lakini wamekuwa hawana majibu kamili. Tumewauliza uko wapi udongo waliotoa kwenye mashimo haya ili tuurudishie japo nasisi tupate raha ya kuishi kwenye tambalale kama ilivyokuwa wao hapo zamani, lakini cha kushangaz hata udongo hawajui ni wapi waliuweka. Tumepata mafunzo kadhaa kutoka hukoo dunia yenye tambalale kuwa hapo mwanzo nchi hii ilikuwa tambalale, na ilipendeza kwa kila aliyeitizama. Watu kutoka magharibi walikuja kutazama maajabu ya Nchi hii, hawa Babu zetu hawa, wakatumia mema ya Nchi hii ili kujinufaisha wao, tumepata taarifa kuwa kulikuwako na mawe yenye thamani kubwa kiasi kwamba jiwe moja lingeweza kusomesha watoto wengi kuanzia chekechea mpaka Elimu ya juu. Nayo tumeuliza hawajui tena yalipo, na cha kushangaza zaidi hatujui mawe yale yaliyochimbwa yameleta faida gani katika kaya zetu” aliongea kijana mmoja huku akiwaacha midomo wazi wageni wale kutoka mataifa ya nje ambao walikuja kufuatilia chimbuko la sauti kutoka kwenye mashimo iliyokuwa ikisikika inasema MEA CULPA MEA CULPA MEA MAXIMA CULPA.
Basi kwa ghafla wazungu wale walijikuta tayari wamezungukwa na kundi lile la watu huku wakiwatembezea kichapo cha hatari, wazungu wale waliomba radhi kwa watu wale walioonekana kuwa ni wenye hasira kali, basi na wao kwa uchungu walianza kuimba maneno waliyokuwa wakiyatamka wazee wale “MEA CULPA MEA CULPA MEA MAXIMA CULPA”. Kwa huzuni sana alisimama mzee mmoja kati ya wale waliokuwa wakiadhibiwa na kusema…………
“vijana wapendwa naomba mnisikilize, ni kweli tumekosa na tumekosa sana, kiasi cha kushinda masaa 24 tukisujudu mbele yenu huku tukiimba MEA CULPA MEA CULPA MEA MAXIMA CULPA, yaani NIMEKOSA MIMI NIMEKOSA MIMI NIMEKOSA SANA,ila hao wageni mngewaacha ila nao wakaongee na babu zao wawajulishe kuwa kile walichotushauri kimesababisha leo hatuishi kwa Amani” alisema Mzee Yule na kuendelea kusujudu pamoja na wenzake.
Hakika maneno ya Mzee Yule yalionekana kuwa ni ya busara sana, wageni wale waliamriwa kuondoka ili wakawapashe habari babu na bibi zao walichokikuta kule. Wageni wale waliondoka huku wakiwa wanamaumivu makali sana, wote walienda kuwaonyesha wake zao Alama za mijeredi wake zao huku wakiendeleza kusambaza ukweli juu ya Nchi yenye Mashimo yanayoongea.
Na L.A.MUGISHA.


Comments